MMEPEWA BURE TOENI BURE
Hili neno kwa wengi
wakilisikia basi hujua kuwa ni mafundisho ya kutaka sadaka, maana ndivyo
linavyotumika mara nyingi tunapokuwa makanisani.
Mmepewa vyote bure na
toeni bure ni tabia ya Mungu wetu yaani kuwapa wanadamu neema kwa kila jambo
(mfano wokovu, rehema, baraka). Hakuna kati ya wanadamu anayestahili mambo
hayo, tunapewa bure tu. Hivyo Mungu anatutaka na sisi tuwe kama yeye maana
tumeumbwa kwa mfano wake na sura yake (mwanzo 1:26-27, zaburi 82).
Wanadamu wengi tunaogopa
kupoteza mali au vitu vya thamani kwa kuwapa watu wengine. Kwa wasiwasi kwamba
kesho tutaishi kwa taabu, lakini wakati mwingine Mungu anatupa afya njema bure
ili tuwahudumie wenye maradhi, anatupa mali nyingi ili tusaidie wahitaji (zaburi82:3-4).
Mungu anatubariki bure kwa vyeo ili tusaidie wanaoonewa na kupokonywa haki zao
(zaburi 82:3).
Japo kwa jinsi ulimwengu
ulivyo tufundisha tunasaidia watu ili waje kutusaidia baadae (hapo tunasaidia
watu wa karibu/wanaojiweza/wenye nafasi nzuri ili nasisi watukumbuke na
watusaidie kwa nafasi zao. Isipotokea tunayotarajia tunajikuta katika hali ya
uadui, kuchukiana, vinyongo na wivu katika mioyo yetu. Hii inafanya Marafiki
zetu wawe wanaojiweza kiuchumi/maarufu/au wenye mamlaka kubwa pengine wenye
mavazi na afya nzuri (mithali 19:4,6,7)
Anaetoa vipawa ni Mungu
hivyo kila kipawa tulicho pewa bure lazima kitolewe bure (mathayo 25:14-15,
waefeso 4:7-). Pia ni vema kuheshimu kipawa cha mwingine na vipawa vyetu nikwa
faida ya jirani zetu wote tunaotakiwa kuwapenda kama nafsi zetu (1wakorintho
12:4-11, 2wakoritho 8:1-15,). Mara nyingi ulimwenguni jirani zetu ni watu wetu
wa karibu (mume au mke), wazazi, ndugu, watu wa dini/dhehebu tofauti na sisi,
watu mashuhuri, maskini, rangi/kabila tofauti, wenye tabia njema na wenye tabia
mbaya machoni petu. Wote tuwapende kama nafsi zetu.
Kwa wale ambao ni
watumishi wa Mungu yaani wale walioteuliwa na kristo Yesu ili kumtumikia (waefeso
4:11). Tunatakiwa kujua katika kuurithi ufalme wa mbinguni lazima tufanye kazi
zote alizotupa maana mwamuzi/hakimu wetu atakuwa ni Kristo mwenyewe. Yeye
atatupa hesabu yote kama tunahaki ama hatuna haki ya kuurithi ufalme wake uliowekwa
tayari tangu kuumbwa kwa ulimwengu. Tusije tukasema Bwana kwa jina lako
tulihubiri na tulitoa pepo lakini atasema siwajui ninyi na akawaita wale wenye
haki nakusema “njooni mliobarikiwa na Baba yangu, Urithini ufalme mliowekewa
tayari….. kwa maana nalikuwa na njaa, mkanipa chakula; nalikuwa na kiu,
mkaninywesha; nalikuwa mgeni, mkanikaribisha; nalikuwa uchi, mkanivika;
nalikuwa mgonjwa, mkaja kunitazama; nalikuwa kifungoni mkanijia” (mathayo 25:34-36,
mathayo 7:21-23).
Kwa kupewa bure maisha
ambayo tunasema mazuri basi tunanafasi ya kutoa bure pia. Hasa kwa wale wenye
mahitaji na matatizo au shida ambao hata kurudisha fadhira ni ngumu. Maana
Mungu hutufanyia hivyo, akitupa vitu vyote kwa neema tu na hata kurudisha
hatuwezi. Mungu anataaka tuwe kama Yeye. Ndio dini ya kweli hiyo.
Hivyo tunapopewa mali
nyingi au vyeo vikubwa na kuvikumbatia ili visipotee na kuwa na hofu ya kuibiwa
au kunyang’anywa matokeo yake ni presha, tension, stress pengine kuanza kuwa na
Imani kwa waganga, wachawi na mambo kama hayo. Wengine hujikuta katika ibada za
makaburi.
Maoni
Chapisha Maoni