NENO KATIKA MOYO NA KATIKA KINYWA


Moyo
Tulivyojifunza awali kuwa moyo ni sadaka ya pekee naya muhimu kumkabidhi Mungu yaani toba (isaya 57:15, zaburi 32:1-5). Hata hivyo kwa moyo mtu huamini, kwani Imani ya mtu huwa moyoni mwake (warumi 10:10). Pia ni vema kujua kuwa uhusiano wa Mungu na mtu hujengwa moyoni kupitia njia ya Imani kwa Yesu kristo (warumi 5:1-11). Siku zote Imani ya mwanadamu kwa Yesu kristo hudhihilisha upendo wake kwa Mungu, hivyo Imani humpendeza Mungu, na upendo huo wa kweli ndio sheria iliyo kuu naya kwanza kufuata (yohana 6:29, kumbukumbu 6:5)
Neno Katika Moyo
Tukumbuke kuwa Mungu ni Roho nao wamwabuduo katika kweli humwabudu katika Roho na kweli. Tafsiri ya neno roho na moyo katika maandiko ya biblia takatifu yanashabihiana. Na mahali pengine huonyesha kama roho huwa ndani ya moyo wa mtu. Pia tukumbuke tunaposema Roho maana yake ni neno la Mungu yaani injili ya kweli inayo ambatana moja kwa moja na Roho mtakatifu ambae ni Mungu (yohana 1:1, yohana 6:63, 1 wathesalonike 2:8, yohana 5:38)
Kumbe basi moyo wa mtu ukitawaliwa na neno la Mungu na kuithibitisha Imani ya kweli katika kristo Yesu mtu huyo huwa na mahusiano makubwa na Mungu (yohana 14:23). Japo watu wengi hudhani kusemasema kwamba wanampenda Mungu na wanaimani na Yesu, wakati mioyo yao ikijua dhahili kuwa wayasemayo si kweli ila ni kuwalaghai watu na kuwatapeli ili wakidhi matakwa yao tu, hii ni kujidanganya, wasijue kuwa wanamtumikia ibilisi, na kujipalia makaa ya hukumu kichwani, maana Mungu huchunguza mioyo (mathayo 24: 24, zaburi 78:36-37, yeremia 17:10, ufunuo 2:23)
Mtu ambaye moyo wake hautawaliwi na maneno ya Mungu basi mwovu humtawala kirahisi (matendo 8:18-24, waefeso 2:1-4). Na mwovu hudhani kuwa vile amemtawala mtu basi ni rahisi kutawala wengine, kitu ambacho hatoweza kukifanya kwa mtu anae mwamini Yesu kristo katika Roho na kweli (mathayo 4:1-11, luka 10:18-20, mathayo 5:48,)
Moyo wa mtu hutawaliwa kwa neno, na maneno mtu ayasemayo yanatoka katika moyo wake (Luka 6:45) Mungu ni Neno (yohana 1:1) na neno la Mungu ni Roho (yohana 6:63) na tukilishika neno la Mungu ndipo Roho wake huja na ndani ya mioyo yetu na kututawala na kuishi nasi (yohana 14:23-24)
Neno Katika Kinywa
Basi neno litokalo kinywani mwako ni kiashiria kikubwa kuonesha kama moyo wako unatawaliwa na Mungu au na ibilisi au pengine na hisia zako za mwili (ayubu 22:22) Na kama ukitaka kuijaribu roho kwa mtu anayedai kuwa anamwamini Mungu ni kwa kupitia meneno ya kinywa chake (mathayo 15:18) hivyo tusipende kuamini kila roho.
Unajisi na haki ya mtu hutokana na maneno yake. Siku zote limtokalo mtu limeujaza moyo wake (mathayo 15:10-20). Basi kama kwa kukiri tu mtu hupata haki na kwa moyo mtu akiamini hupata wokovu, hivyo neno likitoka katika moyo wenye Imani ya kweli ni jambo jema litokanalo na neema ya Mungu (warumi 10, mithali 18:21)
Karama za Mungu kama wokovu, uponyaji, ulinzi, ukombozi hata ufufuo zinapatikana kama moyo unaamini Yesu katika kweli yote na kwa kinywa unakiri Imani yako kwa kristo (kama moyo wako unatawaliwa na Mungu maneno yako yamekuwa roho)
Tena ni vema kukumbuka katika tafakari hii kuwa kila neno litahukumiwa mbele za Mungu lakini pia kila neno jema litahesabiwa haki (mathayo 12:33-37).

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

UHURU WA MKRISTO

MAHUSIANO NA UPENDO BAINA YA MTU NA MUNGU

SADAKA YA MOYO