KUOMBA NA KUSIKILIZA


KUOMBA
Wanadamu tunalojukumu la kuomba tunapoishi duniani, maombi huwa ya namna nyingi kama maombi ya toba, shukrani, maombi ya sifa au kutukuza wakfu au nadhiri, kuomba msaada, kuomba Baraka au fadhili kama uponyaji, muujiza, kuomba kukilimishwa/kipawa/karama za Roho, suala la kuomba ni ibada ya muhimu  na ni jambo la kila mtu lakini linahitaji kuzingatia  mambo yafuatayo;
Ø Kusali rohoni (yohana 4:23-24)
Kuomba kwa moyo(moyoni) kunasaidia kuomba wakati wote kujizoeza kuomba moyoni ni faida kwa mkristo. Neno linasema ni vema kuomba kila wakati bila kukoma (1 wathesalonike 5:17). Japo inawezekana kuwa ni ngumu kama tumezoea kuomba kwa kupayuka-payuka (mathayo 6:7) tukiamini kwamba Mungu atatukumbuka kwenye shida zetu. Sina maana kuwa ni vibaya kuomba kwa sauti ila nataka kusema kuna wakati wa kuomba kwa sauti maana huwezi kuomba kwa sauti kila wakati na neno linatuhitaji kuomba kila wakati.Neno pia linasema tusijisumbue kwa jambo lolote isipokuwa kwa kusali na kuomba lakini haja zetu na zijulikane (    luka 21:34-36)
Mungu ameufanya moyo kuwa chumba cha siri kwa ajili ya makutanio baina Yake na binadamu. Mtu anapokuwa anaomba moyoni hakuna mtu anayeweza kujua hata awe mwandani wako(mathayo 6:6, luka 7:39, mithali 4:23, )  
Ø Jua haki zako kabla ya kuomba( Daniel 9:7 )
kabla ya kuomba nivema kujua haki zako katika ufalme wa Mungu( mathayo 6:33, isaya 51:1-2 isaya 53 ) haki zetu zinapatikana kupitia Yesu kristo mwenyewe (yeremia 4:2, yohana 16:9-10 zaburi 89:14). Alikufa msalabani ili tupate haki zote za msingi ili tuishi duniani tupate uponyaji, uhuru toka kwenye vifungo vya ibilisi, mahusiano na Mungu baba na tupate Baraka zote, na rehema za Mungu kwa kupitia damu yake iliyomwagika msalabani. Kwa kifupi kila tunachoomba kwa Mungu tunapata kupitia jina, na damu ya Yesu kristo (yohana 14:13-14, isaya 61:1-11). Mungu anajua haja zetu hata kabla hatuja muomba (mathayo 6:8)
Ø Tambua nyakati za kuomba (zaburi 32:6)
Kwa mtu mtauwa anafahamu ni wakati gani wa kuomba, kumbe kuomba si suala la kujisikia bali kabla ya kuomba kuna mambo ya kuzingatia, mtu mtauwa anapaswa kumwomba Mungu pale anapopatikana (zaburi 32:6) na ni kweli tunapo mtafuta Mungu anapatikana (isaya 55:6) pia ni ngumu kumpata Mungu tunapokuwa hatusikilizi nakutii maneno yake ( yeremia 7: 24, isaya 58:9)
Ø Tuombe kwa kuongozwa na Roho wa Mungu
Binadamu wengi hatujui kuomba kwa maana tunaongozwa na matakwa ya miili yetu hivyo hisia na hulka ndo hutuongoza kwenye maombi na sio Roho wa Mungu na matakwa yake. Matakwa ya Roho wa Mungu Ndio hayo hayo matakwa ya Mungu (warumi 8:5-6,26-27,34-39). Mungu ni Roho tunapo muonba lazima tuongozwe na Roho wake na hakikisha Roho wa Mungu anapopatikana ndipo unapo muomba.
KUSIKILIZA
Kuomba ni vema kwa binadamu lakini kusikiliza ni muhimu Zaidi (mhubiri 5:1-6)

Basi tunapofika mbele za Mungu, tunapojisogeza mahali patakatifu pake ili tumuombe inabidi tumsikilize kwanza (waebrania 4:16). Kwa maana Mungu anayajua mahitaji yetu kabla hatujamuomba. Kusikiliza ni bora Zaidi kuliko kuomba vitu tusivovijua (mathayo 20:22, warumi 18:26, mhubiri 5:1). Tena kuomba wakati unaemuomba anajua haja zako na anashughulika na mambo yako, ni sawa na kutomtambua Mungu na kazi kubwa alizofanya kwako. Tuwe wepesi wa kusikiliza maagizo na kutekeleza na hiyo ndiyo Imani na hasa ndiyo pekee inayo mpendeza Mungu (mhubiri 5:1,6, waebrania 11:1) Mungu anatuagiza tumsikilize Yesu maana kwa kufanya hivyo tutaweza kuimalisha Imani zetu (mathayo 17:3,5, mithali 8:34-35). Kumsikiliza Mungu ni muhimu sana ilikujiepusha kuomba vitu vingi na tusivyo vijua au kulaumu na kujihesabia haki mbele za Mungu (luka 18:9-14)

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

UHURU WA MKRISTO

MAHUSIANO NA UPENDO BAINA YA MTU NA MUNGU

SADAKA YA MOYO