IMANI NI KUSIKIA NA KUTII
Maandiko
matakatifu yanatufundisha kuwa imani ni njia pekee ya kufikia Ufalme wa Mungu.
Pasipo imani haiwezekani kumpendeza Mungu (Waebrania 11:6). Sio kwa matoleo ya
sadaka au kuhudumu katika nyumba zetu za ibada ndio tunaweza kumpendeza Mungu,
bali ni kwa imani. Tafsiri ya imani ni kusikia na kutii neno litokalo kwa
Kristo. Hivyo ni jukumu la kila mwanadamu kuamwamini Yesu Kristo ili kuufikia
Ufalme wa Mungu.
Imani
katika Yesu kristo inahusisha mambo makubwa mawili yaani usikivu na utiifu.
Usikivu ni hatua ya kwanza na utiifu ni hatua ya pili katika imani ajabu ni
kwamba haya Yote mawili hufanywa na Yesu kristo mwenyewe na sio kwa nguvu za
binadamu.
1.
Usikivu- ni kusikia neno
litokalo kwa Kristo; binadamu wote walio wateule wanauwezo wa kusikia sauti ya
Mungu na pia wanauwezo wa kusikia sauti ya Yesu kristo (1Yohana 4:6). Basi imani
chanzo chake ni kusikia; na kusikia huja kwa neno la Kristo (Warumi 10:17).
Maandiko matakatifu yanaonyesha awali wana wa israeli (Yakobo) taifa
lililoteuliwa na Mungu walisiishi kwa kusikia sauti ya Mungu, lakini wengi
waliangamizwa na wengine kupelekwa utumwani kwa sababu ya kutotii neno lake
yaani sheria Yake (Warumi 10:18, Mathayo 4:4). Ndiyo sababu Yesu kristo
alitumwa ulimwenguni ili kila ayasikiaye na kuyatii maneno yake asipotee bali
awe na uzima wa milele (yohana 14:24)
2.
Kutii – ni kutekeleza yale
maagizo yaliyo sikiwa kwa matendo. Kama ilivyo kuwa hatua ya mwanzo wa imani ni
kusikia na hatua ya pili ni kutii. Basi anayeweza kulitii neno la Mungu
ameitimiza imani yake na imani yake huwa kamilifu (Yakobo 2:21-22). Binadamu
wanauwezo wa kusikia lakini wachache sana au hakuna wanaoweza kulitii neno la
Mungu. Kwa sababu awali baba yetu Adamu alishindwa kulitii neno la Mungu.
Ndomana Mungu mwenyewe aliamua kwa kupitia Yesu kristo imani yetu ianzishwe na
itimizwe (waebrania 12:2).
Sasa
imani huanzishwa na Yesu na inatimizwa na Yeye mwenyewe, na binadamu wanatakiwa
kufahamu kuwa utimilifu wa imani katika Yesu kristo hauji kwa uwezo wa mwili
bali kwa Roho mtakatifu. Wengi wanafahamu Yohana alibatiza kwa maji lakini Yesu
Kristo anabatiza kwa Roho mtakatifu na kwa moto(Luka 3:16).
Adam
hakuweza kutii neno la Mungu kwa maana yeye aliongozwa na tamaa za mwili; Kuja
kwa Yesu kristo kulifanya imani yetu ianze maana yeye alikuja duniani akauvaa
mwili kama wana wa adamu wengine lakini pia kwa kuongozwa na Roho mtakatifu
aliishinda dhambi, kuzimu na mauti. Na ndiye aliepaingia patakatifu pa Mungu na
katika hekalu takatifu akafanywa kuhani mkuu wa milele ambaye kwa mwili wake
alifanya sadaka takatifu ya kufuta dhambi(Waebrania 10). Hii inadhihirisha kuwa
Yesu kristo alikuja kurejesha uhusiano baina ya Mungu na wanadamu ambapo
binadamu aliokolewa kwa mkono wa Mungu ikiwa neema na huruma zake zinatumika
kutengeneza imani kama njia ya kumfikia na si kwa kuhesabiwa haki kwa matendo
ya sheria (warumi 3:21-31).
Imani
inampendeza Mungu na hii imekuwa njema kuliko sadaka au matoleo yaliyokuwa
yanatolewa awali katika tamaduni za Israel (1 Samweli 15:22). Na pia imani yetu
ni katika Yesu kristo wote wamwaminio hulisikia na kutii neno lake, kwa kufanya
hivyo hukombolewa na kuimarishwa katika imani (Luka 6:46-49)
Yesu
kristo ndiye awezaye kujalia wanadamu kutii neno la Mungu; tukimwamini nakuomba
kwa toba na unyenyekevu kwa Baba kwa njia yake tutapewa Roho mtakatifu (Matendo
2:38) maana Yesu ni kuhani mkuu habatizi kwa maji tu bali kwa Roho
anayetuwezesha kutii neno la Mungu.
Imani
humwezesha mtu kupokea baraka na nguvu za Mungu na kuuona utukufu wake (Marko
5:25-34,Yohana 11:40). Hivyo hatua ya kwanza ya imani ni kusikia neno lakini
hatua ya pili ni kutii nayo huja kwa ubatizo wa Roho wa Mungu hapo imani
hukamilika na huwa takatifu (Yuda1:20)
Maoni
Chapisha Maoni